Friday, December 17, 2010

STREET CHILDREN IN MWANZA CITY.

By, K, Aloyce.

Street children are increasing day after a day, the causes for them to be high in Mwanza city are due to social and economic aspects such as poverty, urbanization, sickness, divorce, peer pressures, family conflicts, and lack of governmental care for the non- able people in the society. As it is examined briefly bellow here as follows.
Poverty, however the buffaloes of poverty knock the children away from their families due to the fact that, according to United Nations Development program (UNDP) report, Tanzania is the 4th poorest Country from the bottom in the world. So, children tend to escape the life in their families moving into streets expecting to get relief from their families’ hard life. Hence this habit has produced a lot of street children in Mwanza city.

Divorce, this is a second factor where by it has been proved that in every  ten (10) street children, six (6) of them came to live in streets because they found it to be more peaceful than living with their step parents,  in their blended families where they lack a genuine parental care. That is why the number of children continues increasing almost every day.

Death & diseases, High mortality rate caused by incurable diseases such as HIV/AIDS, has been another caused of the influx of Street children in Mwanza City.
A quite large number of children who are currently moving into street run away from their guardian’s families to escape harsh treatment from the members of their guardian’s families after they have lost their parents.
Peer pressures, in some cases, children find it difficult to resist the influence from other children of their age who are in streets. Already so some of the street children originate from good and rich ferrules regardless their difficult life in streets. Most of these children are disobedient to their strict parents so they run away from their families to seek freedom of life styles for instance taking alcohol and smoking. 
Family conflicts, un maintained large families lead to the destruction  of the pillars of  a family hence alcohol distraction and lack of peace in the family accelerate children to find a helping hand, love and peace in street. Parents of children have to be careful in their families so as to avoid unnecessary conflicts.
Urbanization, Since Mwanza is the backbone of the Tanzania’s economy because of its rich in natural resources and it’s high population, there is a rapid movement of children from rural areas to Mwanza Urban centers to search for wages and other related tasks so that they can get anything to feed their stomatches.
However, street children face a lot of problems in the city, the following are some of the problems facing the street children personally in their daily life in Mwanza city.
Lack of basic needs, the homeless street children sleep along the corridors in Mwanza town. They are not sure of their food and clothes; many die of malaria and others transmitted diseases because no one cares for their health.
Drug abuse, Street children find themselves involved in the non- medical use of drugs that has always been interfering with their healthy and productive life. Some of the drugs used by these children include cocaine, marijuana, heroin and petrol, as illegal drugs and alcohol, tobacco, inhalants and prescription drugs as legal drugs. Children often have a sense of invulnerability on drugs regardless their age or sex claiming to get energy or help them relax. Children use drugs to seek relief of the stress of life in streets because they have no hope for their future and sometimes they fail to get food and tend to eat in damps, Regardless of why children abuse drugs, many continue the practice because they become dependants (addicted) on drugs.
Homo sexuality, in street it is common for an elder street boy to play fornication with another young boy whom they call “Their wives” Other children (boys) under this immoral practice have decided to make it a business with adults of the same sex whom in return they give them a little amount of money or  food. Similarly young girls are being raped and some bear children unexpectedly. So some tend to throw their born children away, some abort and others get into prostitution in return for payment to save themselves and their children.
The society is affected by presence of large number of street children who cause the insecurity of people in public transport vehicles, in the streets to mention the most common.

REFERENCE
Street children around
Rufiji street
in Mwanza city.
Body sellers (sexual intercourse oriented) at Vitunguu near with
Pamba Road
, Mwanza city available on the place every day at 8:00 pm.
Miss Bora (Shangazi) near Aspen Hotel in Mwanza city.


WANAWAKE KWANZA, JE?, WANAUME.

Mwanamke yeyote aishie hapa duniani ni kiumbe dhaifu sana, akiliyake haipishani nay a motto mdogo. Ndiyo maana hata serikali za nchi nyingi zimeweka widhara ya wanawake na watoto kwa kumlinganisha mwanamke na watoto wadogo. Chakushangaza sasa hivi nchi zenye mbilikimo wa siasa na wenye mipango lukuki ya kupokonya hela za kodi za wananchi zimeamua kuwapa nafasi wanawake nyazifa za juu sana serikalini bila kuona kuwa ni hatari sana kwa taifa.

Kwaufupi ni kwamba, mwanmke ni kiube ambaye hafai kabisa hata kidogo kuendesha huduma za jamii, mfano mzuri ni wa Bwana YESU wakati anachagua mitume wake 12 hakuthubut kumchagua mwanamke kwa sababu aliona kuwa kutakuwepo na matatizo ya rushwa, tamaa a ngono, wivu, ufuska, ufisadi, na kadhalika. Hii inatukumbusha tu kuwa tumesahau tulikotoka hivyo tunahribu tunakokwenda.

Kitu kingine cha kuzingatia hapa ni Mateso aliyoyapata Samsoni yalitokana na usaliti wa mkewe ajulikanye kwa jina la Delila. Haiwezekani hata kidogo kumweka mwanamke mbele kusimamia chombo cha umma.

Kifo cha Rwanda Magere “the rock” kilisababishwa na mwanamke ambaye alijitoa mhanga kuolewa na huy shujaa, kasha kumdadisi siri zake zote na kuwaambia watu wa nyumbani kwao jinsi ya kuweza kumuua, na kweli walifanikiwa kumuua kwa kushambulia kivuli chake.

Dhambi ya asili tuliyoirithi kutoka kwa Adamu na Eva ilisababishwa na udhaifu wa mwanamke ambae ni HAWA (EVA) kukubali kula tunda walilokuwa wamekatazawa kulila na mwenyezi Mungu. Hicho ndicho kilimfanya Adamu awe kwenye wakati mgumu sana wa kujibu maswali toka kwa Mungu hadi akaanza kujikanyaga kwa kuukwepa ukweli na kumrushia mkewe kuwa “mke uliyenipa ndiye kaniletea hilo tunda  na ndipo tukalaaniwa na sisi ambao hatujashiliki kulila hilo tunda na hatujui linafananaje.

Je, ni wangapi wanaopoteza mwelekeo wa maisha kwa sababu ya mwanamke? Je, ni mambo mangapi yameharibika hapa duniani kwa kusababishwa na mwanamke? Ni mengi na hayana maelezo mafupi. Kwa sababu hata kuenea kwa ukimwi kunasababishwa hasa na watoto wa kike kwa kuvaa nguo zenye kuleta matamanio yaani ziko fupi sana na zenye kubana maumbile kupita kipimo.

Mwisho msomaji napenda nikuambie kuwa, ukikuta serikali yoyote imeegemea sana kuwapa nafasi za juu wanawake ujue ni serikali ya kifisadi na maamuzi yake huwa yanategemea sana mwamke nyumbani kasema nini. Ni serikali yenye viomgozi ambao ni mbilikimo wa fikra za kulipeleka Taifa pazuri. Ni serikali yenye kuingia mikataba mibovu na yenye kusimama kusimamia kesi na kuishia kushindwa huku ikihukumiwa kulipa mabilioni ya fedha. Ni serikali ya watu masikini wa akili wasioweza kufanya mambo yao wenyewe bila kuomba misaada. Serikali za aina hizi ni za nchi za Afrika.

Sunday, December 12, 2010

KARUGENDO NAKUKUBALI

UKIMWI: Uaminifu huvunjika mara nyingi kuliko kondomu zinavyopasuka!

BAADA ya Baba Mtakatifu kubadilisha msimamo wake juu ya matumizi ya kondomu, wasomaji wangu wameniomba niandike makala juu ya msimamo mpya wa Baba Mtakatifu. 
Nafikiri sina jipya; maana mimi msimamo wangu bado ni ule ule. Nilisema ni suala la wakati, na sasa bahati nzuri wakati umetimia mapema tukiwa bado hai na tumeweza kushuhudia!
Lakini Askofu Methodius Kilaini anataka tuamini kwamba Baba Mtakatifu alinukuliwa vibaya. Hayo ni matatizo yake binafsi! Baba Mtakatifu amenena na  dunia imemsikia! Nami narudia kusema yale yale niliyoyasema miaka mitano iliyopita….
Ni ukweli usiopingika kwamba maadili ya ngono yalikuwapo kabla ya ukimwi. Hata hivyo maadili haya hayakutusaidia kuukwepa ukimwi; kwa kuwa watu waliyakaidi kwa sababu kadhaa.
Kwa kuangalia hali halisi ilivyo sasa, inaelekea kwamba watu wataendelea kuyakaidi maadili ya ngono mpaka hapo sababu zinazowafanya kuyakaidi zitakapoondoka. Kanuni ya u-Machiavelli inatawala leo kuliko kanuni nyingine yoyote kadri maadili ya ngono yanavyohusika!
 Ziko sababu kadhaa zinazowafanya watu kuwa wafuasi wa Machiavelli. Kwa kuangalia mitindo na maisha ya watu kingono, ziko sababu kama saba hivi zinazowasukuma kuabudu itikadi hiyo. Nitajaribu kuorodhesha kwa ufupi.
Mtindo wa kwanza unahusisha kundi la watu wanaofanya ngono kwa sababu tu ni anasa. Kila  mlango wa fahamu tulionao wanadamu unatupa anasa kwa namna fulani. Kunusa manukato, kuonja asali, kutazama sinema, kusikiliza muziki, na kufurahia mwanga wa jua la asubuhi kwa kutumia neva zilizo kwenye ngozi ya miili yetu, zote ni anasa za mwili.
Anasa ya ngono inapatikana kupitia neva za ngozi ya mwili, na kwa njia ya mzunguko kupitia milango mingine yote ya fahamu. Uhusiano wa kingono hapa ni wa muda tu. Kama zilivyo anasa nyinginezo.Hakuna anasa ya kudumu!
Pamoja na ukimwi kuzagaa, mtindo huu wa maisha bado umeshika mizizi. Ni mtindo unaomgusa karibu kila mtu asiye kuwa na kasoro ya kimwili. Ili kuubadilisha mtindo huu wa maisha, panahitajika juhudi za pekee zikiambatana na ushirikishwaji, majadiliano, elimu, uwazi, imani ya kweli na maisha ya pamoja. Ni vigumu kuubadilisha mtindo huu wa maisha kwa kuukemea kama wafanyavyo wenye nguvu za kukemea pepo wabaya!
Mtindo wa pili unahusisha kundi la watu wanaofanya ngono kwa sababu wanataka kuzaa mtoto. Hawa, mara nyingi, ni wanawake ambao hulazimika kufanya ngono pale tu wanapojisikia kupata mtoto. Ni nani atahusika katika kusababisha mimba hiyo, ni suala la kuamua tu siku hiyo.
Baada ya mimba kupatikana kila mmoja anaendelea na maisha yake. Akihitajika mtoto wa pili, atatafutwa mtu mwingine kwa utaratibu huo huo. Utaratibu huu unaendelea.
Hawa, japo uhusiano wao ni wa muda, hawatatumia kondomu kama kizuia-magonjwa. Hii ni kwa sababu kondomu hiyo hiyo pia ni kizuia-mimba; wakati wao wanahitaji mimba itungwe!
Pamoja na janga la ukimwi, mtindo-maisha wa aina hii bado unaendelea kushamiri.Pia ni vigumu kuubadilisha mtindo huu wa maisha kwa kuukemea tu bila kufanya kazi ya ziada.
 Mtindo wa tatu unahusisha kundi la watu wanaofanya ngono kwa sababu wanataka usalama wa kijamii maofisini, makanisani, mashuleni, vyuoni na hata ikulu. Kwa mfano, mwanafunzi mmoja anayeyaweza mambo kidogo darasani anaweza kujenga urafiki wa kingono na mwenzake kama namna ya kumweka karibu rafiki yake ambaye anaamini anaweza kumsaidia kusoma vizuri.
Jambo kama hili linafanyika katika biashara, kwenye siasa na maofisini kati ya wakubwa wa kazi na watu walio chini yao. Hata kwenye baraza letu la mawaziri tunasikia kwamba ngumi zinapigwa. (Kwa mfano, inasemekana kwamba mawaziri wawili wa kike walipigana kwa ajili ya kigogo wa juu katika serikali yetu). Uhusiano wa kingono hapa ni wa muda tu. Pamoja na ukimwi kushamiri, mwenendo huu unazidi kushamiri hadi leo.
Mtindo wa nne unahusisha kundi la watu wanaofanya ngono kwa sababu tu wanatafuta kutambulika kwa wenzao kundini. Kundi laweza kuwa kikundi cha kusoma pamoja chuoni, au kikundi cha makuli, au kikundi cha wavuvi, au kikundi cha walimu katika shule fulani, au madaktari katika hospitali fulani, au hata kikundi cha vijana wa rika za kuchumbiana (courtship age).
 Hawa wa kundi la kuchumbiana wanahangaika kutafuta kuolewa na mtu ambaye amekwisha kujijenga kiuchumi. Njia pekee ambayo wamechagua ni kutoa rushwa za ngono kwa watu wengi wengi tu, mpaka hapo atakapojitokeza mwenye nia ya kuoa, lakini aliyejijenga tayari!
Kitu kimoja ambacho nimegundua hapa ni kwamba, inawezekana kabisa kuna mtu anayemzimia msichana ili kumwoa, na msichana pia anatamani kuolewa na huyo bwana. Lakini ugunduzi wangu ni kwamba, msichana huyu akishatokea kufanya ngono na mtu fulani hata kama alikuwa hampendi sana, kuliko yule wa kwanza ambaye anajifanya mwana maadili, huyu mwanamaadili anasahauliwa! Baadaye, msichana anatelekezwa. Safari hii inaendelea! Mwenendo huu unaendelea kushamiri pamoja na kwamba janga la ukimwi lipo.
Mtindo wa tano unahusisha kundi la watu wanaofanya ngono kwa sababu wanataka kuonyeshana upendo (affection) au shukrani. Kwa kawaida kama unampenda mtu unampa zawadi. Na zawadi nzuri ni kumpa mtu kile kitu anachokipenda. Kitu kitakachomfurahisha.
Watu wengi wanapenda anasa, na hasa anasa ya ngono. Hivyo, kumpa mtu hiyo anasa ni namna ya kuonyesha upendo au shukrani. Mwenendo huu bado unaendelea pamoja na kwamba ukimwi umezagaa.
Mtindo wa sita unahusisha kundi la watu wanaofanya ngono kwa sababu za kimapato. Hawa hujihusisha na ngono kama tendo la mabadilishano yanayohusisha vitu kama vile  pesa, gari, kiatu kizuri, nguo za bei mbaya, au mshahara mzuri!
Mabadilishano huweza kuhusisha pesa, mali au huduma nyingine yoyote. Kinachofanyika kati ya mhudumu wa baa na mnywaji wa pombe baa ndicho hicho hicho kinachofanyika kati ya bosi ofisini na katibu wake, tangu ofisi ndogo ndogo kama vile bucha ya nyama mpaka ikulu! Ma-Sugar Daddy na ma-Sugar Mummy ni mafundi wa kutoa zawadi za magari.
Bosi ofisini huweza kumpa mtu aliye chini yake ruhusa ya kuondoka ofisini kila Ijumaa saa sita mchana, badala ya saa kumi na nusu, ili mradi tu mtu huyo awe tayari kutoa penzi kadri bosi wake anavyotaka.
Ikiwa kuna maeneo ya kupaki kwa ajili ya vigogo wa ngazi za juu kwenye kampuni, mtu wa chini, hata kama ni mfagiaji, atapata sehemu ya kuegesha gari lake ilimradi tu awe tayari kutoa anasa ya ngono kwa bosi mhusika.
Yako matukio mengi ya aina hii. Na pamoja na ukimwi, bado tabia hii inashamiri. Na kibaya zaidi makuwadi wakuu wa tabia hizi ni baba na mama zetu, wajomba na shangazi zetu, na watu wengine wa rika za kati kwenda juu, kwa kuwa hawa ndio tayari wana nyenzo za udhibiti (power resources) kwenye makampuni haya.
 Mtindo wa saba unahusisha na unapaswa kuhusisha kundi la watu wanaofanya ngono kwa utaratibu unaohusisha sababu zote nilizozitaja hapo juu. Kusudi hili liwezekane, watu hawa wanaishi pamoja kama mke na mume katika ndoa.
Kwao, penzi linapaswa kuwa ni zawadi! Kwa kawaida ukishampa mtu zawadi, iwe kalamu au nguo, ni yake. Huwezi kumnyang’anya. Vivyo hivyo ukishajitoa kwa mwenzako kama zawadi huwezi ukajinyakua na kujitoa kwa mwingine.
Kwa tafsiri ya namna hii, hawa watu wanapaswa kujenga uhusiano wa kudumu kabisa. Mtindo-maisha wa aina hii ndio “unaopigiwa debe” na viongozi wengi wa dini.
Watu katika kundi hili, kwa sababu za kimantiki, hawatarajiwi kujihusisha na ngono za kupokezana (relay sex). Lakini, kwa masikitiko makubwa kabisa, watu katika kundi hili ndio wanakata mbuga na kujiingiza katika mitindo maisha mingine iliyotajwa hapo juu. Pamoja na ukimwi, bado ukataji mbuga unaendelea asubuhi, mchana, jioni na usiku wa manane kama kawaida!
 Kwa msingi huu, nafikiri kwamba, wakati watu wanaendelea na itikadi ya u-Machiavelli, ni bora kuwasaidia kwa mbinu yoyote inayowezekana, kama vile kondomu mpaka hapo watakapouacha u-Machiavelli!
Watu wakiacha u-Machiavelli, hata kondomu zitakosa soko! Izingatiwe kwamba jambo la msingi si kuzuia matumizi ya kondomu. Jambo la msingi ni kuwaelimisha watu wabadilishe maisha yao.
Na hii si kwa kuhubiri na kutunga sheria nyingi nyingi; bali ni kwa kuyagusa maisha yenyewe kwa kushirikiana na jamii nzima.
Ziko mbinu nyingi za kuweza kuwafanya watu waache imani ya ki-Machiavelli. Lakini kwa maoni yangu, mahali pa kuanzia ni kutokomeza itikadi mbovu ya mfumo dume (patriarchy)!
Kanisa Katoliki ni kinara wa mfumo dume. Limechangia kiasi kikubwa kuendeleza na kuutukuza mfumo dume. Linaishi na kutenda kana kwamba wanawake si watu!
Uongozi wote, maamuzi yote ya kanisa hata na maamuzi yanayowahusu wanawake moja kwa moja, kama uzazi wa mpango,utoaji mamba yanaamuliwa na wanaume.
Mfumo dume ni hatari kubwa katika vita ya kupambana na UKIMWI, kama Kanisa Katoliki linataka kutoa mchango wake katika vita hii ni lazima liupige vita mfumo dume. Ni vigumu watu kuupiga vita mfumo dume wakati wanaoana viongozi wao wa kiroho wanaukumbatia mfumo huu wa kinyanyasaji.
 
Mitindo-maisha hii yote inafanana katika jambo moja kubwa: ngono za kupokezana (relay sex) ambapo mwanamke ni kama mawimbi ya sauti ambayo huruka toka mnara mmoja hadi mwingine! Hii imekuwa ni kanuni ya maisha ya wanawake wengi leo, na hasa wale wa maofisini.
Kwa sababu ya itikadi hii mbovu, siasa za kijinsia (sexual politics) zinatawaliwa na wanaume. Hii inatokana na nguvu za kiuchumi walizonazo kwa msaada wa mfumo dume. Kutokana na itikadi ya mfumo dume, nyenzo za udhibiti kiuchumi (economic power resources) ziko mikononi mwao.
Nyenzo hizi ziko mikononi mwao kutokana na itikadi mbovu ya kutukuza mfumo dume. Kwa upande mwingine, wanawake wanazo nyenzo za udhibiti wa kingono (sexual power resources)! Hizi nyenzo wanapewa kwa msingi wa maumbile yao.
Katika mazingira haya ambapo itikadi mbovu ya mfumo dume imemfanya mwanamume kuwa na nguvu za kiuchumi, lakini ikamwacha mwanamke akiwa ametelekezwa, japo anazo nyenzo za udhibiti kijinsia, sasa mwanamke anajikomboa kupitia nyuma ya pazia! 
Kinachotokea sasa hivi ni kama kuna sumaku mbili zinazovutana: sumaku ya kiume yenye nguvu za kiuchumi, na sumaku ya kike yenye nguvu za kingono. Mwanamme anapata anasa ya ngono, mwanamke anapata anasa ya ngono na gawio la kiuchumi kidogo.
Itikadi ya mfumo dume imekuwa na athari kubwa kwa sasa, kiasi kwamba kila mwanamke anataka kuuza “huduma ya ngono” kwa sababu ni njia ya haraka ya kujikomboa.
Hata wale waliobahatiwa kupata elimu nzuri kabisa, bado akili yao imenasa katika tope hili la mfumo-dume. Bado wanatumia miili yao kama ngazi, badala ya kutumia akili na maarifa yao waliyoyapata.
Na kibaya zaidi ni kwamba, mwenendo huu unazo baraka zote za wazazi wote ambao nimewatafiti kwa njia zangu, baadhi yao wakiwa ni washauri wangu. Baadhi ya wazazi hawa ni wazee wa makanisa, wenyeviti wa mabaraza ya maparokia, maprofesa, na hata mawaziri!
Hawa hawa ni washauri wa karibu wa mapadre na maaskofu wetu. Ninapata shida kufikiri juu ya jambo hili! Nahisi kila mtu ni mnafiki leo!
Mheshimiwa Askofu Kilaini amekuja na mpya, anasema: Tuone soo! Je, tuone Soo kwa ngono tu? Mbona yako mengi. Nimeelezea juu ya mfumo dume na matatizo yake. Mbona Askofu Kilaini asiseme tuone soo  juu ya mfumo dume?
Ukimwi umeenea zaidi kwa sababu ya mfumo dume. Hivyo haitoshi kuwataka watu waone soo bila jitihada ya kubadilisha mifumo. Mambo si rahisi kama anavyoyachukulia Askofu Kilaini.
Kama uaminifu unavunjika kuliko kondomu zinavyopasuka, si ni vyema kutengeneza kondomu zilizo imara zaidi hadi kuhimiza matumizi yake hadi pale watu watakapoelemika na kujikomboa juu  ya umaana na umuhimu wa  tendo la ngono?