Monday, January 31, 2011

JE, AHADI HIZI ZA WAGOMBEA ZINATEKELEZEKA?

Na ALOYCE KALUNDE
Ahadi za Kikwete:
  1. Kujenga reli mpya kutoka Dar es Salaam mpaka mikoa ya Kanda ya ziwa-Nzega, Tabora
  2. Mkoa wa Tanga kuwa Jiji la Viwanda- Tanga mjini
  3. Tabora kutumia maji ya Ziwa Victoria-Igunga
  4. Kulipa madeni ya chama cha Ushirika mkoa wa Shinyanga (SHIRECU)- Shinyanga
  5. Kumaliza migogoro ya Ardhi nchini- Dodoma
  6. Wakulima kuacha kutumia jembe la mkono-Dodoma mjini
  7. Kuwapatia trekta wakulima -Kata ya Mrijo, Dodoma
  8. Wananchi kutoondolewa kwenye Ranchi ya Misenyi-Kagera
  9. Kujenga Uwanja wa Ndege Misenyi-Kagera
  10. Kupanua Uwanja wa Ndege Bukoba-Bukoba Mjini
  11. Kujenga uwanja wa ndege mkubwa Kigoma - Kigoma Mjini
  12. Mtukula kupatiwa umeme kutoka Uganda- Kagera
  13. Mikoa ya Kagera, Kigoma, Lindi, Rukwa na Ruvuma kuunganishwa katika gridi ya taifa ya umeme- Kagera
  14. Kuimarisha Takukuru kwa miaka mitatu-Kagera
  15. Hukumu kwa waliopatikana na hati ya kuua albino- Mbeya
  16. Kununua meli kubwa kuliko MV Bukoba-Kagera
  17. Kuanzisha benki ndogondogo kwa ajili ya wajasiriamali
  18. Serikali kuvisaidia vyama vya ushirika-Mwanza
  19. Kuimarisha usalama Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika kwa kupeleka kikosi maalum chenye vifaa kupambana na wahalifu-Mwanza
  20. Wilaya ya Geita kuwa hadhi ya mkoa Januari mwakani- Geita
  21. Kulinda muungano kwa nguvu zote-Pemba
  22. Kuwajengea nyumba waathirika wa mafuriko Kilosa-Morogoro
  23. Kununua meli mpya kubwa Ziwa Nyasa-Mbeya mjini
  24. Kujenga bandari Kasanga –Rukwa
  25. Kumaliza tatizo la walimu miaka mitano ijayo - Songea
  26. Kufufua mgodi wa makaa ya mawe Kiwira -Mbeya
  27. Kuzuia hatari ya kisiwa cha Pangani kuzama- Tanga
  28. Kununua bajaji 400 kwa ajili ya kubeba wajawazito hasa vijijini- Iringa
  29. Kujenga barabara yenye kiwango cha lami kutoka Same mpaka Kisiwani –Kihurio na kuiunganisha na barabara kuu ya Moshi -Dar es salaam- Same mkoani Kilimanjaro
  30. Kumaliza tatizo la maji katika wilaya ya Same-Same Mjini
  31. Kuboresha barabara za Igunga -Tabora
  32. Kusambaza walimu 16,000 katika shule za sekondari zenye upungufu makubwa wa walimu- Kisesa Magu
  33. Kununua vyandarua viwili kwa kila kaya- Mbeya Mjini
  34. Kuzipandisha hadhi hospitali maalumu saba nchini kuwa za rufaa ili kuipunguzia mzigo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MHN)-Hydom Manyara
  35. Kulinda amani nchini kwa kuzuia chokochoko za kidini, kikabila na kisiasa- Musoma
  36. Kulinda haki za walemavu- Makete
  37. Kujenga baabara ya Njombe- Makete kwa kiwango cha lami,urefu wa kilomita 109- Iringa mjini
  38. Kujenga barabara Musoma–Mto wa Mbu Arusha-Arusha
  39. Kuanzisha jimbo la Ulyankulu- Shinyanga Mjini
  40. Kujenga barabara ya lami Manyoni-Kigoma– Kaliua,Tabora
  41. Kukarabati barabara ya Arusha Moshi-Arusha Mjini
  42. Kuboresha barabara ya Handeni, Kondoa,mpaka Singida-Dodoma
  43. Kuwafidia wanakijiji ng’ombe waliopotea wakati wa ukame mwaka 2009- Longido 45.Vijiji vyote vilivyoko kilomita 15 kutoka kwenye bomba kuu la mradi mkuu wa maji wa Ziwa Victoria-Shinyanga-Kahama kuunganishiwa maji - Shinyanga
  44. Tatizo la umeme kufikia kikomo Novemba mwaka huu mkoani Arusha –Arusha mjini
  45. Kukopesha wavuvi zana za kilimo-Busekera, Wilaya ya Musoma, .
  46. Kuwapatia maji wakazi wa Wilaya ya Longido- Longido
  47. Kujenga barabara ya lami kupitia pembezoni mwa Hifadhi ya Taifa ya Seregenti – Ngorongoro
  48. Utekelezaji wa mpango wa maendeleo ya kilimo kuwasaidia wafugaji kuweza kupata na kutunza mifugo yao vizuri- Mbulu mkoani Manyara
  49. Kusambaza maji nchi nzima-Babati vijijini
  50. Kusambaza umeme, utoaji wa huduma za afya, na uboreshaji wa kilimo cha umwagiliaji na utoaji ruzuku kwa wakulima. mwaka 2010-2015-Babati vijijini Kuongeza mara tatu idadi ya wananchi wanaonufaika na ruzuku ya pembejeo za kilimo kwa mfumo wa vocha.-Iringa
  51. Kuhakikisha Isimani inapata maji ya uhakika- Iringa
  52. Kuiwekea lami barabara inayokwenda katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, ambayo ndiyo hifadhi kubwa kuliko zote Tanzania-Iringa
  53. Kulinda usalama wa wananchi kwa ujumla ili kudumisha amani na sifa ya nchi-Ifunda
  54. Kutokomeza malaria 2015-Bunda,mkoa wa Mara
  55. Kuwapa wanawake nafasi zaidi-Kilolo ,Iringa
  56. Kuisadia Zanzibar kuendeleza miradi mbalimbali ya kijamii-Kibandamaiti Mjini Zanzibar
  57. Kuipandisha hadhi hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar kuwa ya rufaa-Kibandamaiti mjini Zanzibar
  58. Kuisaidia Zanzibar kila panapohitajika msaada-Kibandamaiti
  59. Serikali kujenga upya bandari ya Mbambabay-Ruvuma
  60. Ununuzi wa Meli mpya yenye uwezo wa kubeba tani 400-Mbambabay Ruvuma
  61. Kufufua chama kikuu cha ushirika cha wakulima wa Mbinga(MBICU) –Ruvuma
  62. Ahadi Rais wa Marekani Barack Obama kuimwagia misaada TanzaniaRuvuma
  63. Ahadi hakutakuwa na umwagaji wa damu baada ya uchaguzi-Dar es Salaam
  64. Mtwara kuwa mji wa Viwanda –Mtwara
  65. Ahadi ujenzi wa kwanda cha dawa ya kuua viluilui vya mbu-Kibaha
  66. Hospitali ya Tumbi kuwa ya mkoa-Kibaha
  67. Halmashauri ya manispaa ya Kibaha kutenga eneo maalumu la viwanda -Kibaha

Ahadi za Dk W. Slaa:
  1. Kujenga nchi isiyo na ufisadi.
  2. Kurejesha maadili ya taifa, na utumishi wa umma.
  3. Kuanza mchakato wa katiba mpya ndani ya siku 100.
  4. Kufufua Tanganyika ili irejee mezani kujadili muungano na Zanzibar.
  5. Kufufua uchumi wa Nchi kwa kutumia rasilimali zilizopo
  6. Kukata asilimia ishilini (20%) ya mshahara wa rais.
  7. Kupunguza mishahara ya wabunge kwa asilimia kumi na tano (15%).
  8. Kuweka Mwenge wa Uhuru Jumba la Makumbusho.
  9. Kutoa huduma bora za afya bure.
  10. Kutoa elimu bure chekechea hadi kidato cha Sita (elimu ya lazima)
  11. Kufuta kodi ya vifaa vya ujenzi
  12. Kuwalipa wazee wa EAC fedha zao ndani ya siku 100
  13. Kuwalipa wanaoidai DECI
  14. Kubana matuzi ya serikali.
  15. Kupunguza ukubwa wa serikali (Mawaziri 15, manaibu watano).

Ahadi za Profesa Lipumba
  1. Elimu ya bure kuanzia msingi hadi chuo kikuu
  2. Kubana matumizi kwa kupunguza ukubwa wa baraza la mawaziri
  3. Kuunda serikali shirikishi
  4. Kusimamia rasilimali
  5. Kuimarisha miundombinu
  6. Kusimamia na kuboresha afya
  7. Kuboresha kilimo, viwanda na uwekezaji
  8. Kurudisha chakula cha bure mahospitalini

MSHINDI WA UCHAGUZI 2010

Rais Jakaya Kikwete
Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilal
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda

WIZARA NA MAWAZIRI WAKE:

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
1.Utawala bora, Mathias Chikawe
2.Mahusiano na Uratibu, Stephen Wassira
3.Menejiment ya Utumisi wa Umma – Hawa Ghasia

Ofisi ya Makamu wa Rais
4-Muungano-Samia Suluhu Hassan
5-Mazingira - Dk. Terezya Luoga Hovisa

Ofisi ya Waziri Mkuu
6.Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvi
7.Uwezeshaji na Uwekezaji, Dk. Mary Nagu

8) Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, George Mkuchika
Manaibu: Aggrey Mwanri na Kassim Majaliwa

9) Wizara ya Fedha, Mustapha Mkullo
Manaibu: Gregory Teu na Pereira Ame Silima

10) Wizara ya Mambo ya Ndani-Shamsi Vuai Nahodha,
Naibu: Balozi Hamis Kagasheki

11) Wizara ya Sheria na Katiba: Celina Kombani

12) Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa: Bernard Membe
Naibu: Mahadhi Juma Mahadhi

13) Wizara ya Ulinzi na JKT: Dk. Hussein Mwinyi

14) Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi: Dk. Mathayo David Mathayo
Naibu: Benedict Ole Nagoro

15) Wizara ya Mawasiliano Sayansina Tenknolojia: (Prof. Makame Mnyaa Mbarawa
Naibu: Charles Kitwanga (mawe matatu)

16) Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof. Anna Tibaijuka
Naibu: Goodluck Ole Madeye

17) Wizara ya Maliasili na Utalii: Ezekiel Maige

18) Wizara ya Nishati na Madini, William Ngeleja,
Naibu: Adam Malima

19) Wizara ya Ujenzi: John Magufuli
Naibu: Prof. Harrison Mwakyembe

20) Wizara ya Uchukuzi: Omary Nundu
Naibu: Athuman Mfutakamba

21) Wizara ya Viwanda na Biashara Dkt. Cyril Chami
Naibu: Lazaro Nyalandu

22) Wizara ya Elimu: Dk Shukuru Kawambwa
Naibu: Philipo Mulugo

23) Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii: Dk. Hadji Hussein Mpanda
Naibu: Dk. Lucy Nkya

24) Wizara ya Kazi na Ajira: Gaudencia Kabaka
Naibu: Dkt. Makongoro Mahanga

25) Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto: Sophia Simba
Naibu: Umi Ali Mwalimu

26) Wizara ya Elimu Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo: Dk. Emmanuel Nchimbi
Naibu: Dk. Fenella Mukangara

27) Wizara ya Ushirikiano EAC, Samuel Sitta
Naibu: Dk. Abdallah Juma Abdallah

28) Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Prof Jumanne Magheme, Naibu: Christopher Chiiza

29) Wizara ya Maji, Prof Mark Mwandosya
Naibu: Eng. gerson Lwinga

Kabla ya kutangaza, Rais Kikwete alisema haya:

Katika Muundo wa Serikali hakuna mabadiliko makubwa isipokuwa yafuatayo:
1.Idara ya Umwagiliaji tumeiunganisha na Kilimo ambako ndipo ilipokuwa zamani.
a.Imeonekana upangaji wa maendeleo ya kilimo unakuwa hauna hakika bila ya umwagiliaji kuwa sehemu ya kilimo. Tuliihamishia maji kurahisisha pia upangaji na hasa kwa vile maji ndiyo wanaotoa haki ya matumizi ya maji.
b.Kwa kuwa tatizo la uhaba wa maji ya binadamu ni kubwa sana na tunataka tuongeze kasi ya kukabiliana na tatizo hilo tumeona tuiondolee wizara hii mzigo wa umwagiliaji ili ibaki na kazi moja tu ya kuhakikisha kuwa watu wanapata maji safi na salama mita 400 kutoka wanapoishi.
2.Idara ya Vijana tumeihamisha kutoka Wizara ya Kazi na kuihamishia Wizara ya Habari kwa sababu kuu 2.
a.Kwanza inashabihiana na michezo na utamaduni.
b.Tunataka Wizara ya Kazi ipate muda wa kutosha wa kushughulikia masuala ya ajira na wafanyakazi ambayo sasa yamepanuka.
3.Shughuli za Uwezeshaji wa Wananchi zilizokuwa Wizara ya Fedha na Wizara ya Kazi zitahamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu.
4.Marekebisho mengine ni madogo:
a.Katika Ofisi ya Rais tunairudisha shughuli ya mahusiano na jamii hivyo tunaongeza Waziri wa Nchi ambaye pia atashughulikia shughuli zilizopanuka za Tume ya Mipango, MKURABITA na TASAF.
b.Katika Ofisi ya Waziri Mkuu tutakuwa na Waziri wa Nchi wa kushughulikia Uwekezaji na Uwezeshaji wa Wananchi.
c.Katika Ofisi ya Waziri Mkuu Wizara ya TAMISEMI tumeongeza Naibu Waziri wa kushughulikia masuala ya Elimu.

WALIAPISHWA
Jumamosi tarehe 27 Novemba, 2010 saa 05:00 asubuhi.

Swali langu ni je, ushindi huu ulikuwa halali?, kwanini NEC inasingizia baadhi ya softwares za wapiga kura kupotea?

No comments:

Post a Comment